Je Shetani yupo?

Mwandishi: 
Pasi Palmu
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Biblia inazunguamzia juu ya shetani, ijapokuwa kwa nadra. Yeye si sawa wala kinyume na nguvu za Mungu. Yeye kiumbe cha Mungu. Sababu zilizopo shetani kuwa mwovu kwa asili zinaonekana kuwa sababu zilizosababisha mwanadamu kuanguka: Kiburi, tamaa ya kuwa sawa na Mungu. Kwa sababu Mungu alikuwa na mapenzi mema kuhusu uumbaji wake na kwenda kinyume na mapenzi yake ni uovu kabisa. Hivyo shetani kila hali ya kumpinge Mungu.

Shetani anashughulikaje? Biblia inafundisha kwamba anafanya kazi ndani ya watu wasiotii” kama hatufuati mapenzi ya Mungu, tunafuata mapenzi ya adui wa Mungu na hivyo kuwa katika himaya ya shetani. Hata hivyo tunaweza kubadilisha msimamo kwa kumkiri Yesu kuwa Bwana na Mwokozin wetu.

“Vaeni silaha za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za shetani kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama, bali ni juu ya ufalme na mamlaka, juu ya mkuu wa giza, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho”
(Waefeso 6:11-12 SUV)