Nawezaje kuwa Mkristo? Nawezaje kutoa maisha yangu kwa Yesu?

Mwandishi: 
Sirkka-Liisa Huhtinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Kila mkristo anaushuhuda wake jinsi alipata kumjua Yesu. Mmoja aweza kupata mafunuo usiku, mwingine ilimchukuwa miaka mingi kupta kuamini na mwingine alimjua Yesu tangia utoto wake. Hakuna ushuhuda uliyomzuri kuliko wa mwingine. Hata hivyo nini kiliwafanya wawe wakristo kwa pamoja ni kwamba Bwana Yesu alifungua mioyo yao kupokea imani.

Hapa kuna ushauri mdogo kuhusu wale ambao wanaotaka kujua jinsi ya kuwa Wakristo: Acha kutoka kutoka kwa Mungu. Fungua masikio na sikiliza nini Bibilia inafundisha. Angalia yale Yesu amefanya kwa ajili yako. Mungu anakupenda. Yesu alikufa msalabani kwa ajili dhambi zako. Wewe ni mpendwa wa Mungu wako. Amini tu na mshukuru Mungu.

Unaweza kuomba: ”Yesu mwana wa Mungu nihurumie mimi mwenye dhambi”. Kulingana na Biblia Mungu atasikia maombi yeko na atakusamehe dhambi zako zote.Amehahidi kukusamehe katika Yesus Kristo.

Imani si kuhusu hisia ni kuhusu kuamini katika moyo kwamba Yesu ameniokoa. Muhimu ni kwamba unamwamini nani. Yesu atakuokoa. Wokovu ni zawadi kutoka kwa Mungu. Kwa imani tunapokea zawadi hii.

Kama umebatizwa umekuwa muumini maana umerudi nyumbani tena na kuwa na uhusiano na Mwokozi wako. Tafuta Kanisa pale utasikia msamaha wa dhambi na kushiriki Meza ya Bwana na wakristo wengine.

Yesu anawaita kwake kila mmoja uwe umebatizwa au hujaptizwa, katika ubatizo tulisafishwa na kuunganishwa na Wakristo wengine.

(Nini kitatokea kama sikubatizwa?)

“Kwa kuwa kila atakaye liitia jina la Bwana ataokoka.”
(Warumi 10:13 SUV)

Ombi: - Bwana Yesu kristo mwana wa Mungu unirehemu mimi mwenye dhambi.