Yesu ni nani?

Mwandishi: 
Sirkka-Liisa Huhtinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Haya ndiyo Wakristo wa kwanza walikiri. Waliamini kwamba Yesu ni mwana wa Mungu aliyekuja duniani kama mwanadamu. Kuna kifungu kinachosema “Yesu ni Bwana” kinadhaihirisha hakika imani yao.

Injili ndani ya agano jipya zinatuambia habari njema kuhusu Yesu, jinsi alivyochukuliwa mimba kwa uwezo wa Roho mtakatifu na kuzaliwa na bikira Maria, na jinsi alivyoishi, kufundisha na kutenda miujiza mingi. Yesu ni nani, mateso yake, kifo chake na kufufuka kwake siku ya tatu viko katika msingi wa Ukristo.

Je! Yesu ni nani kwako?
Ufahamu wako juu ya Yesu, na yeye ni nani kwako inaamua hali yako umilele. Kwa hiyo ingiza mikono yako katika bibilia na tafuta kujua zaidi.

Kwa kufa kwake msalabani kwa ajili ya dhambi zetu, na kufufuka kwake kutoka kwa wafu, Yesu alifanya njia kwetu ya kumfhamu katika wenyewe. Ni kupitia Yesu tu tunaweza kuokolewa na kuwa na uhusiano na Mungu.

“Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.”
(Matendo ya mitume 4:12 SUV)