Biblia inafundisha juu ya dhambi isiyosamehewa, kumkufuru Roho Mtakatifu - Hii ina maana gani?

Mwandishi: 
Ville Auvinen
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Wakati wasomi wanapinga kwamba Yesu alifanyakazi kwa kupitia nguvu za shetani, Yesu aliwaonya kuhusu kumkufuru Roho Mtakatifu. Kumkufuru Roho mtakatifu ni dhamira ya kinyume ya kazi za Roho Mtakatifu. Kuna mifano mahali pengine katika Biblia pia, katika barua ya kitabu cha Waebrania anazungumzia dhambi ya dhamiri ambaye ina kupelekea katika utengano na Mungu. Kwa njia hii haizungumzia dhambi nyingine ila ni dhambi inayokufanya ukatae imani.

Maneno ya Yesu katika waraka kwa Waebrania usieleweka kama kushutumu mtu yeyote lakini kama onyo kwa wale wote ambao hawajafanya dhambi hii. Ni muhimu kukumbuka kwamba mlango wa Mungu upo wazi kwa kipindi hiki ambacho injili ya Yesu Kristo inahubiriwa. Na shida kwa mtu ambaye alifanya dhambi ya kukufuru Roho Mtakatifu kwamba Mungu atasamehe au la! Lakini haya ni kutokuwa na mapenzi kumrudia Mungu – Moyo umefanya mgumu. Kwa hiyo yeyote anayeogopa kutenda dhambi ya kurudia anaweza kuwa na hakika kwamba hajafanya hiyo dhambi kwa sababu toba ni alama ya moyo ambao bado unaskiliza wito wa Mungu.

“Naye mtu yeyote atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa na katika ule ujao.”
(Mathayo 12:32,SUV)