Nini kinatokea kwetu wakati tutakufa?

Mwandishi: 
Pasi Palmu
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Mwanadamu aliumbwa kwa kuishi milele. Kuvunja mapenzi ya Mungu kifo kikaja, na hakika kinatuhumiza sisi sote. Hata hivyo kifo hikitashinda mwisho.

Katika kifo, muda wetu wa rehema unafika mwisho. Katika ulimwengu huu ulioumbwa tunaweza kuishi kwa zawadi ya Mungu. Hata kama hatumjali Mungu kabisa. Kinachotokea, hata hivyo, wakati tunapoteza pesa zetu, uzuri, nafasi zetu katika kazi, afya na maisha? Nini kinatokea tunapokutana na Mungu aliye uchi katika dhambi zetu? Yeye aliyetupa uzima atatuuliza tumeutumiaje? Hatutakuwa uchi katika kipindi hicho. Biblia inatufundisha kwamba katika imani tutavikwa mavazi meupe, nayo ni haki ya Kristo. Tuliopewa katika ubatizo. Katika ni imani, inamilikiwa.

Nini kuhusu baada ya kufa? Waliokufa wamelala Kiroho kabla ya ufufuo wa siku ya mwisho? Biblia inatufundisha kwamba katika kifo mtu anakwenda katika ukweli mwingine. Sio lazima kujua urefu wa kipindi hicho, lakini kipindi hiki cha kusubiri ni cha furaha au cha huzuni au wakati wa dhiki. Dhamiri ikiwa nzuri kila mmoja anajua nani anasubiri, ni vizuri kusubiri.

“Lakini ndugu , hatutaki msifue habari zao waliolala mauti , msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini maana ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye."
(1 Thesalonika 4:13-14, SUV)