Injili ya Yohana sura ya 2 – Moto wa Mungu unaenezwa

Mwandishi: 
Erkki Koskenniemi
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Arusi ya Kana 2:1-12

Hadithi ya muujiza wa kwanza ambao Yohana anazungumzia haupatikani katika injili nyingine tatu. Tukio hili lilipatikana katika mji wa Galilaya,sehemu ambayo haijulikani kwetu sisi.

Matukio haya yalitokea huko mashariki ya kati iliyojumuhisha pia chakula halisi. Mvinyo uliwaishia, lakini Yesu aliwaambia wale vijana waliokuwa arusini wajaze mabalasi yenye lita mia 600 maji kuwa mvinyo wa hali ya juu. Yohana anasema kwamba wanafunzi waliona utukufu wa Yesu na wakamwaamini.

Hadithi hii inatufundisha nini? Katika agano la kale mvinyo ulikuwa na maana sana. Sehemu ya maajabu ya wokovu uliotolewa kwetu na Mungu unajumuhisha wingi wa sherehe (Mwanzo 49:8-12). Wakati Yesu anaokoa sherehe ya arusi Kana, Yohana aneleza kwa hakika hivi: Kuna mwokozi mkuu mwenye uwezo katikati ya watu wa Mungu.

Maana nyingine: hii mara kwa mara haijadiliwi: Ni mwonekano wa Yesu juu ya vijana maarusi na kusherehekea kwao juu ya arusi. Hata hivyo aliwaita watu wengine kuacha kila kitu nyuma na kumfuata yeye, hakuwa na maana kudharau familia, ilikuwa ni kinyume chake familia hupokea Baraka yake.

Tunapaswa pia kujadili mafundisho ya Biblia kuhusu kunywa mvinyo. Ni wazi kabisa ulevi ni dhambi, lakini Biblia haijadili kabisa kutokunywa. Kabisa huu ni mtindo wa nidhamu na mzuri tena unaokubalika, lakini haupaswi kudaiwa kwa kila mmoja. Ni kama kingo mbili za geti “njia nyembamba sana” ambayo imewekwa katika huu mtindo” kila mmoja katika ndhamira yake apime kwa uzito ni ni upande gani wa njia anatembea. Ni kosa makubwa kutenda juu ya dhamira ya mtu mwingine.

Jambo la kuongezea: Yohana na mafanano

Wakati mwingineni vigumu kuweka Injili ya Yohana pamoja injii zingine tatu. Hii inatoka katika mfano wa hadithi ambayo Yesu anasafisha hekalu: Wainjilisti wote watatu wa kwanza wanasema kuhusu Yesu akitembea Glilaya, safari yake kuelekea Jerusalemu, na kifo chake na ufufuo wake. Katika maelezo yao, na hadithi ya Yesu kusafisha hekalu imewekwa katika siku ya mwisho ya maisha ya Yesu. Lakini Yohana anatoa muda tofauti. Yesu alifika Yerusalemu mara nyingi, na pia kipindi cha pasaka, hivyo alifanya huduma yake wazi miaka mingi. Usafishaji wa hekalu uliwekwa na Yohana mapema kipindi cha huduma ya maisha ya Yesu.

Wasomu wengi wanatofautiana kuhusu injili ya Yohana inaamini zaidi ya zingine Inawezekana kwamba Yesu alifundisha kikundi kidogo cha wanafunzi wake kwa muda mrefu kuliko watu wengine wote baada ya wao kuondoka. Yeye Yohana alikuwa na kusudi kuweka tukio hilo katika hatua za mwanzo kabisa katika huduma za Bwana Yesu. Kwa sababu hiyo hakuna hata mmoja anaweza kukosa kusema kuwa Yesu alikuwa kiongozi wa kisiasa tu.

Hata hivyo, wainjilisti wote wane wameelezea juu ya kusafishwa kwa hekalu, vizuri kama walivyoelezea juu ya mateso yake na kufufuka kwake. Injili si historia ya maisha iliyoandikwa kwa mpangilio na utaratibu wa maisha ijapokuwa zimehifadhi taarifa kamili na sahihi ya historia. Kusudi la Injili ni kutufanya sisi kumwamini Kristo. Ushuhuda wa Wainjilisti wane, achilia mbali mawazo yao, ni ya utajiri na mengi ya maelezo mazuri kuliko yangeandikwa na mwaandishi mmoja.

Yesu anasafisha hekalu 2:13-25

Nyakati zile za mwanzo sawa na sasa hivi, kusanyiko la watu ndani ya hekalu uliweka mazingira mazuri ya kibiashara. Omba omba walikuwa na sehemu yao. Na Wayahudi walikuwa na sehemu ndogo hekaluni ambayo waliweza kutoa dhabihu kwa Mungu. Wale waliokuja na nia ya kutoa dhabihu walitakiwa kujigharamia malazi na chakula na wanyama kwa ajili ya dhabihu. Ushuru wa hekalu uliweza kufanya kwa hela maalumu kwa thamani ya pesa ya kiyahudi, hata hivyo walikuwa ni sehemu yao. Makaburi ya makuhani wakuu yalionyesha maisha ya kitajiri ya makuhani waliotumika kutoa huduma. Si ajabu kuona kwamba umuhimu wa hekalu ulisahaulika.

Kusafisha hekalu ulikuwa wa lazima na Yohana na injili zingine waliyaandika haya. Yesu aliwafukuza wafanya biashara wote ndani ya hekalu. Walifanya sehemu takatifu kuwa sehemu ya wanyanganyi. Wayahudi walilijua vizuri Agano la kale na waliyajua vema maneno ya nabii Malaki:

“Angalieni, namtuma mjumbe wangu, naye ataitengeneza njia mbele yangu; naye Bwana mnayemtafuta atalijilia hekalu lake ghafula; naam, yule mjumbe wa agano mnayemfurahia, angalieni, anakuja, asema BWANA wa majeshi. Lakini ni nani atakayestahimili siku ya kuja kwake? Au ni nani atakayesimama atakapoonekana yeye? Kwa maana yeye ni mfano wa moto wa mtu asafishaye fedha, ni mfano wa sabuni ya mtu afuaye nguo; naye ataketi kama asafishaye fedha na kuitakasa, naye atawatakasa wana wa Lawi, atawasafisha kama dhahabu na fedha; nao watamtolea BWANA dhabihu katika haki. Wakati ule ndipo dhabihu za Yuda na Yerusalemu zitakapopendeza mbele za BWANA, kama katika siku za kale, na kama katika miaka ya zamani."
(Malaki 3:1-4, SUV)

Kitu kingine cha muhimu maandiko ya Agano kale yanapatikana katika Zaburi ya 69:9 (“Maana wivu wa nyumba yako umenila, Na laumu zao wanaokulaumu zimenipata.”).

Majibu ya Yesu kwa Wayahudi yalikuwa kama upuuzi tu, kila aliyesikiliza alifikiri kuwa Yesu anazungumzia juu ya hekalu la kawaida, lakini yeye Yesu alikuwa akizungumzia juu ya mwili wake mwenyewe. Kwa ajili hiyo kifo cha Yesu na ufufuo wake utaleta mtazamo uliopo katika Injili. Tunatazama hivyo hivyo ulinganifu na Marko Masihi kama ni fumbo. Kristo alielezea ukuu wake waziwazi lakini watu hawakuelewa maneno yake.

Wakati wa matukio yaliyoandikwa katika Yohan-miaka 46 baada ya ujenzi wa hekalu-kwa ajabu kwa undani na kwa msaada wake tunaweza mwaka wa Pasaka. Ujenzi wa Helaku ulianza 20/19 KK. Kama ujumbe huu ni sahihi mwana unaweza ukawa 29 au 30.

Katika mistari ya mwisho ya kitabu cha Yohana tunakutana na waswali juu ya sababu ya miujiza. Yesu alifanya miujiza iliyopelekea watu wamwamini. Kwa jinsi hii miujiza ndani ya injili ya Yohana una umuhimu mkuu. Kwa wakati mmoja, mwinjilisti anaongoza utafiti wa Yesu ambao unaiweka imani ya mwanadamu katika nafasi maalumu, Yesu akuwekeza kwa mwanadamu kwa sababu alifahamu imani ya binadamu kuwa legevu.