Injili ya Yohana

Mwandishi: 
Erkki Koskenniemi
Mtafsiri: 
Emmanuel Sitta Samwel

Injili ya Yohana (Biblia Swahili Union Version)


Utangulizi wa Injili ya Yohana

Kwa kuongezea zaidi katika Injili tatu zinazofanana (sinoptiki) za maandiko. Pia Agano Jipya linajumuisha Injili ya Yohana, ambayo inachukuliwa kama dogo (isiyo ya zamani) kabisa katika Injili. Pia inachukuliwa kuwa ni injili iliyo tofauti kabisa na Injili zingine.

Nani aliandika Injili ya Yohana? Vyanzo vya mapema vinamtaja Yohana ndiye mwandishi, "Mtu wa kale wa Kanisa la kwanza". Askofu wa Asia Ndogo, Polykrates (190), anasimulia juu ya Yohana, "ambaye aliegemea kifua cha Mungu na akawa kiongozi wa kinga, shahidi na mwalimu ambaye sasa amepumzika katika mji wa Efeso". Polykrate alizaliwa takriban miaka ya 125 na alikuwa na ujuzi mkubwa juu ya mapokeo ya Asia Ndogo (sasa inajulikana Anatolia). Kulingana na Polykrates, Yohana aliyetajwa hapo juu sio mtume (tofauti na yeye anasema ni kesi na Filippos ambaye yeye pia anasema).
 Kwa mujibu wa Eirenaiosi (Irenaeus), pia Yohana "mwanafunzi wa Bwana ambaye pia alijiunga na kifua chake alijenga injili yake mwenyewe wakati akiishi Efeso katika Asia Ndogo". Eirenaiosi haimwita Yohana huyu kuwa mtume.
 Inaonekana kwamba karibu 130, Askofu wa Hierapolis aliwataja Yohana wawili: "ambao ni Andrea au Petro alisema, au Philippo, au Thomas au Jacob, au Yohana au Mathayo au ni yeyote kati ya wanafunzi wa Bwana alisema, au Aristioni au Yohana wa zamani, ambaye ni mwanafunzi wa Bwana". Inasemekana Yohana wa kwanza alikuja kuwa mtume badaye "pia Yohana wa zamani alikuja kukumbukwa baadaye na watu wa zama za sasa.

Hata hivyo, kwa mujibu wa Injili ya Yohana, Yohana alitegemea sana mamlaka ya Kanisa la kwanza ambalo lilijitahidi kujiweka karibu na Petro na hata kuwa juu yake.

Injili ya Yohana na waraka Yohana 1-3 (pia na sehemu ya Ufunuo) ina mambo mengi sana ya kawaida, na ni rahisi kufikiri kuwa yameandikwa katika utamaduni unaofanana sawa na maandiko ya Yohana, ingawa ni hatari sana kukalili kuwa yameandikwa na mwandishi mmoja. (lakini katika Ufunuo hakuna uwezekano huo). Hata hivyo, baraka hizo zinafunua kwamba kulikuwa na uharibifu wa mafundisho, ambayo wao huguswa nayo sana.

Injili ya Yohana ni injili iliyo ndogo zaidi kuliko injili zingine. Na kwa utamaduni wa kawaida imekuwa ikidhaniwa kwamba Yohana alijua sana kutumia maandishi ya watangulizi wake. Dhana hii labda ikawa sahihi, ingawa wasomi wengi wa leo wanafikiri kwamba Yohana hakuwa anajua kuhusu injili pacha (Sinoptiki). Hata hivyo kuna mambo mengi ya kawaida, ingawa Yohana anayatumia tofauti (m.f. utakaso wa hekalu mwanzoni mwa shughuli za Yesu, Yohana 2: 13-16; ukiri wa Petro, Yohana 6: 67-71; upako wa Bethania, 12: 1-8; maajabu ya kushangaza kuhusu muujiza wa samaki, 21: 1-14).

Kwa mujibu wa wainjilisti wote, shughuli za Yesu zilianza katika vitongoji vya Yohana Mbatizaji. Marko na wandishi wengine wa injili pacha wanaelezea jinsi Yesu alivyofundisha kwanza Galilaya na mazingira yake, kisha akaendelea na safari yake ya kutisha kwenda Yerusalemu. Katika Injili ya Yohana, Yesu anarudi kutembelea tena Yerusalemu mara nyingi (2:13; 5: 1; 7:10). hivyo, shughuli zake zinaelezewa kwa kipindi cha muda mrefu sana (Yohana anazitaja sikukuu tatu za Pasaka: 21:13; 6: 4; 11:55).

Hakika kutoka katika utangulizi wake, injili ya Yohana ni kazi imara ya kitheolojia. Mambo kadhaa hufunua hili; mazungumzo yote (Yesu na Nikodemo, Yohana 3) na hadithi za miujiza (k.m. kuwaponya vipofu, Yohana 9), na bila shaka mateso ya Kristo. Yohana anaunganisha Hukumu ya Mwisho (5: 28-29; 12:48) na hivyo huitwa "eskatologia ya sasa" kwa pamoja: ambaye amempata Yesu, amekwisha kuletwa kutoka kifo kwenda uzimani (4:23; 11: 25-26). Ubatizo (sura ya 3) na Ushirika Mtakatifu (sura ya 6) hujulikana, lakini tu kati ya mistari kadhaa.

Sura ya 1-12 inasema kuhusu mambo ambayo Yesu alifundisha,
Sura ya 12-20 inasema juu ya mateso na kifo cha Yesu.
Sura ya 21 ni mambo ya utangulizi.