Injili ya Yohana sura ya 4

Mwandishi: 
Erkki Koskenniemi
Mtafsiri: 
Richard Ondicho Otiso

Yesu na mla watu 4:1-42

Hadithi kuhusu mazungumzo kati ya Yesu na mwanamke msamaria ni ya kufurahisha na ya kupendeza. Kawaida ya injili ya Yohana unajenga matukio ya kutoelewa kwa yule mwana mke. Yesu hata hivyo anakubali kuzungumza naye, na mwisho wa majadiliano si kuwa tu yule mwanamke bali hata raia Wasamaria wanamjia. Hivyo, mwinjilisti anaruhusu watu duni na watu wasio na hekima kuwa lengo la Yesu katika hadithi hii.

Umuhimu wa habari hii kuwa mfano huu inaandaliwa Samaria. Yesu anaondoka Yuda kuelekea Galilaya. Ikiwa mtu angetaka kuvuka ponde la uva la mto jordani ilimlazimu avukie kupitia Samaria. Hii ilikuwa pigo kwa Wayahudi kwa kuwa wao hawakuelewana na wasamaria.

Asili ya Wasamali haikujulikana n ahata sasa inaendelea kujadiliwa kuwa Wasamaria ni mchanganyiko wa watu waloishi Israeli baada ya kuvamiwa katika mwaka wa 722 KK. Wasamaria walijiona kuwa Waisraeli halisi. Lakini Wayahudi waliwachukulia kama wapagani. Kulikuwa na hekalu katika mlima Gerizim ambalo lilipingana na hekalu la Yerusalemu. Wayahudi waliliharibu mwaka wa 128, lakini huo mlima ulibaki mahali maalumu pa maombi. Uhasama kati ya Wayahudi na Wasamaria uliibuka kila mara katika kipindi cha Yesu, na damu ilimwagika wakati wa wasafiri wa Kiyahudi wa Kisamaria walipotofautiana. Wayahudi wa mafundisho sahihi waliwadharau Wasamaria na wakakataa kushirikiana nao. Sasa Yohana anatueleza kuwa Yesu alifanya kinyume lakini alikubalika pale.

Watu wengi ambao wameelezea kisa hiki, wameeleza ni jinsi gani huyu mwanamke anakwenda kisimani katika majira ya saa sita alasiri wakati jua ni kali, na yeye ametoka nje ya mji. Yawezekana hii imefananishwa na yale Yesu anayaona maishani mwake. Huyu mwanamke ni mwenye dhambi ambaye amekataliwa na jamii yake. Ni bora kwa huyu mwanamke angejiepusha na shughuli za kila siku hapo kisimani wakati wanawake wengine walifika kila siku. HivyoYesu alikuwa na kila sababu ambazo zingemfanya asimsogelee, lakini kando na hayo anaanza mazungumzo na huyu mwanamke kitu ambacho kilimshngaza. Katika sehemu za mashariki ya kati, maji ni kitu cha maana, katika mazingira, mazungumzo yanafanyika maeneo ya kisima kikuu ambacho kilichimbwa na Yakobo miaka mingi iliyopita.

Mafundisho ya Yesu kuhusu maji ya uzima ni ya kushangaza. Mwanamke huyu anashindwa kuyaelewa na alikuwa na mawazo kuwa yale maji yaliyokuwa yanaongelewa yalikuwa na nia iliyojificha. Maji ambayo Yesu anazungumzia ni tofauti kabisa. Yesu hayataji lakini msomaji wa injili anaelewa. Yesu anamaanisha mwangaza, ukweli na zawadi ya uhai utokao kwa Mungu. Yeyote anayekutana na Yesu atapata maana kamali ya uhai na hatatamani kitu kingine chochote.

Kama vile manabii wa Agano la kale, Yesu anaangalia kamili ndani ya moyo wa mtu kupitia kwa hadithi hii ya uongo ya Yule mwanamke. Anabadilisha mjadala kutoka kwa maisha yake hadi mahali pazuri na kuingiza mapigo ya zamani: Mungu ataabudiwa wapi, Gerizin au Jerusalemu? Jibu ambalo Yesu analolitoa ni la kawaida kabisa katika injili ya Yohana, sio huko au hapa bali ni katika Roho na kweli. Haya maneno ni kweli tukizingatia uharibifu wa Jerusalemu. Hata wakati hekalu la Jerusalemu lilipoharibiwa bado Mungu alipata kufikiwa kwa maombi. ”Kwa roho na ukweli” - Ni kinyume cha mawazo kuwa ibada ifungwe katika sehemu moja tu. Tunaposoma katika Injili ya Yohana, tunajua inamaanisha kuwa tunapounganishwa na Mwana, Baba hupewa huduma ya kweli, haijalishi msaada unapohitajika.

Hitimizo la mazungumzo yanamalizika wakati Yesu anajitambulisha kwa mwanamke kuwa yeye ndiye Kristo Masihi. Jukumu la mwangaza ulianza palepa.

Wakati yule mwanamke anakwenda na kutorudi na Wasamaria wenzake, ni wakati wa majadiliano. Kiini cha majadiliano ni wakati mwanamke alipoondoka na kurudi. Katika kati ya mazumzo ambayo hayakuwa na uhusiano wa yale ya awali Yesu anaongelea kuhusu kutumwa. Yesu haitaji chakula wanafunzi wake nao walishindwa kuelewa kwa maana chakula chake ni kufanya mapenzi ya Mungu. Kwa vile chakula chake ni kufanya mapenzi ya Baba yake. Baba alivyomtuma mwanawe ulimwenguni na mwana hafanyi chochote ila mapenzi ya baba. Kama vile baba alimtuma mwanae ulimwenguni, mwana anawatuma wanfunzi wake.

Hakuna ukosefu wa kazi wala kukaaka na kungojea. Kungojea kitu kila siku kunahitaji uvumilivu, kupanda na kuvuna. Kilichowaumiza maskini na watu wa kijijini ni njaa na upungufu. Sasa wanafunzi hawakuhitaji taka kungoja. Yesu alikuwa amekwisha kupanda sasa jukumu la wanafunzi ni kuvuna. Maneno hayo siyo yalitumiwa tu wakati ule hata wakat ujao. Kifo cha Yesu na ufufuo wake unapohubiriwa matokeo yake hayatakiwi kusubiriwa hata siku ya hukumu ya mwisho. Yetote atakaye yapokea maneno ya Yesu anamfahamu Mwana na hutoka mautini hadi uzimani. Haya ndiyo yanatokea kwa mwenye dhambi na wale Wasamaria waliodharauliwa.

Imani halisi 4:43-54

Aliporudi Galilaya Yesu alipokelewa kwa heshima kuu (Marko 6:1-6) wakati wa kukataliwa ulikuwa umekwisha.Hivyo kulingana na Yohana alinzia Galilaya na kuweza kutulia kwa kutembelea Yerusalemu. Mfano juu ya mtumishi wa mfalme ambeye alikaa Kapernahumu unatufanya kufikiri kuwa labda umehusiano na mfano ulio katika Matayo 8: 5-15 na Kula 7:1-10 katika misitari hii mazungumzo ni juu ya upanani. Hata hiyo haijatajwa hapa.

Kiini cha maelezo haya ni jinsi huyu afisa ”alivyomwaamini Yesu” . Na majibu ya Yesu kwa huyu mtu aliyekuwa analilia msaada ni kiburi. Yafaa mtu kumwamini Yesu sio tu kwa ajili ya miujiza, ishara au maajabu bali ni kwa neno tu, hata hivyo Yesu anayasema maneno na huyo mtu anayapokea kulingana na neno.

Anaporudi kutoka Kana kuelekea Kaprenaumu, huyu afisa anakutana na watu wanaomletea habari njema, mwanae aliponywa pale tu Yesu alipozungumza maneno yake. Sasa baba yake aliamini pamoja na wale wengine. Kuamini nako kulikuwa na maana tofauti. Hata ikiwa Yohana haelezi, tunaelewa kuwa imani yake inamwangazia ubinadamu wa Yesu.

Hapa tunafundishwa kuhusu ubinadamu wa Yesu na huduma yake. Yesu ni Mwana wa Baba anayetuongoza, kutoka giza kuelekea mwangani kwa uongo hadi ukweli, kutoka kwa kifo hadi uzimani.